Thursday, 30 October 2014

Mganga by Jemimah Thiong'o

Nawatangazia mganga wangu YESU
Ayeyeyeye mganga wa kweli eh
Njoni nyote niwaonyeshe
Mimi nimemwona

Mganga (nimemwona eh)  Mganga (nimemwona)
Mganga wa waganga ni YESU
Mimi  nimemwona
Mganga (nimemwona eh)  Mganga (nimemwona)
Mganga wa waganga ni YESU

Nasema nimemwona  Mganga wa waganga
Anayeinamiwa na waganga wote
Hata na wachawi pia
Wanaleta madawa yao, hata na hirizi
Na wanatangaza maovu yote walotendea wanadamu
Huyu Mganga kazaliwa Bethlehemu
Kalelewa Nazareti
La ajabu ni mwana wa bikira
Nimemwona


Mganga (nimemwona)  Mganga (nimeona Mganga)
Mganga wa waganga ni YESU
Mimi Ye nimemwona
Mganga (nimeona Mganga)  Mganga (Hai Mganga YESU)
Mganga wa waganga ni YESU


Jina la huyu Mganaga kwa kweli lanishangaza
Kwa maana lina nguvu nyingi kama mganga mwenyewe
Lilipotajwa na Petero Tabitha kafufuka
Kiwete njiani akatembea kwa ajili ya hilo jina
Paulo na Sila wakasifu kwa hilo jina
Milango ya gereza ikafunguka kwa jina la Mganga YESU
Nimemwona


Mganga (nimemwona)  Mganga (Hai nimemwona)
Mganga wa waganga ni YESU
Mimi ndio nimemwona
Mganga (nimeona Mganga)  Mganga (Hai Mganga YESU)
Mganga wa waganga ni YESU


Nguo za huyu Mganga hata nazo zina nguvu eh!
Mama aliyevuja damu alipenya katikati ya umati
Kaguza upinde wa nguo damu ikakatika
YESU akamwambia imani yako ndiyo imekuponya
Baada ya kusulubiwa heh! Nguo za huyu mganga
Hazingepasuliwa kwa bei yake zikapigiwa kura
Nimemwona

Heh! Nimeona Mganga
Amebadili maisha yangu
Ukiomba kwa jina lake majabu yanatendeka
Mganga wa kweli
Haiyeyeyye ah

Mganga (Nao wakimbia kwa waganga)  Mganga
 (Njoni Muone Mganga)
Mganga wa waganga ni YESU
Mganga Yesu
Mganga Mganga
(hakuitishi chochote)
Mganga wa waganga ni YESU
(Aliye mganga wangu)
Mganga Mganga
(Ukimwamini anakwambia)
Mganga wa waganga ni YESU
(Aliye Mganga wangu)
Mganga Mganga
(Imani yakuponya)
Mganga wa waganga ni YESU
(Ukimwamini akwambia)
Mganga Mganga
(Enda usitende dhambi)
Mganga wa waganga ni YESU
(Aliye mganga wangu)
Mganga Mganga
(Omba kwa jina lake aliye Mganga wangu)
Mganga wa waganga ni YESU
(Ukiomba kwa jina lake biashara zina nawiri)
Mganga Mganga
(Haya akuongeza imani)
Mganga wa waganga ni YESU










Wednesday, 22 October 2014

Usichoke by Ayzoh Levite





wimbo huu ni wako
baba yangu, mama yangu
kwako dada kijana
eiya nasema

Imepita miaka huku wangoja matokeo
Unajiuliza itakuwa vipi ei
Uliowadhamini wamekuweka kando
Eti kwa sababu hauna chako wewe
Usikate tamaa usiangalie nyuma
Mtazamie Yesu aliye na jawabu lako wewe

Usichoke endelea kungoja tu
Usichoke subiri kidogo mambo yatajipa wewe
Usichoke endelea kungoja tu
Usichoke Mola hachelewi tena
Hana chuki yeye

Bwanangu naomba unitegee sikio lako
Ninayokueleza yasije yakatoka moyoni mwako
Kama yawezekana yaandike vitangani mwako
Ama uyachore kwa wino yasije yakafutika
Huyu Bwana hachelewi wala hananga pupa
Kwa wakati ufaao yeye huja na
Kutekeleza mapenzi yake kwako


Usichoke endelea kungoja tu
Usichoke subiri kidogo mambo yatajipa wewe
Usichoke endelea kungoja tu
Usichoke Mola hachelewi tena
Hana chuki yeye


Usichoke mumy usichoke baba
Usichoke dada
Ndugu yangu usichoke kamwe
Usichoke usichoke Usichoke
Endelea kungoja Bwana wewe

Tuesday, 21 October 2014

Nainua macho yangu by masha mapenzi (psalm 121:1

Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba

Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba


Asema njoo njoo
Asema njoo kwake pumziko
Asema njoo njongea
Asema njoo kwake pumziko
Fadhili zangu ni za milele
Huba langu halina kikomo
Mimi ndimi simba wa Yudah
Mimi ndimi ngome yako


Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba

Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba


Heri awe nawe awe nawe
Heri awe nawe
Mambo yote shwari
Heri awe nawe awe nawe 
Mambo yote shwari
Mikononi mwake
Viumbe vyote vyamtukuza
Mchana kutwa usiku kucha
Yeye ndiye muweza yote
Hakuna limshindalo Mola


Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba

Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba

Nainua macho yangu
Nitazame
Nitazame milimani
Msaada
Msaada wangu weh watoka wapi eh
Ni kwa Baba ni kwa Baba




Wednesday, 1 October 2014

Ni wewe by Zaidi ya Muziki

Shalalalala eya oh shalalalala eya oh
Shalalala eya ooh ooh
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana

Watu wengi wameinuliwa fiti weh
Tena Mungu amewabariki fiti weh
Nina wonder mbona mimi siko fiti weh
Kwani nini nilifanya nina thinki weh
Nimetoa fungu zangu zote kumi weh
Nimetoa hizo zote bila chuki weh
Lakini bado na Baraka hazishuki weh

Nieleze mbona haunigusi weh


Nitazidi kuinua tu(weh) hata mambo yawe aje tu(weh)
Mungu nitakuinua tu(weh) sababu wewe ndiwe Mungu tu

Ni wewe, ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana

Mungu wangu weh wanitosha Ebenezer weh
Ei Mungu wangu weh wanitosha Ebenezer weh
Niliposota hata kuteseka magonjwa nayo yakaniokota
Rafiki zangu wakanitoroka Mungu wangu wewe hukuniacha ha(weh)


Nitazidi kuinua tu(weh) hata mambo yawe aje tu(weh)
Mungu nitakuinua tu(weh) sababu wewe ndiwe Mungu tu

Ni wewe, ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana

Hapa tumefika ni wewe sio kwa nguvu zetu ni wewe
Umekuwa mwaminifu wewe hakuna mwingine kama weh
Maisha ninayoishi mimi ah oh Muziki nayo fanya mimi aah oh
Favour nazopata zote aah oh
Hakuna, hakuna Mungu kama wewe

Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana

Nimepigana vita visivyo Mwokozi nikitumia nguvu zangu
Nguvu sina kama hazitoki kwako
Nasema ni wewe ni wewe wewe weh weiiii
Ooh uwo uwoooo

Nasema ni wewe tunajua ni wewe(nasema ni wewe)
Ninaimba ni wewe kila siku ni wewe
Mzeiya ni wewe Mbuyu ni wewe


Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana
Ni wewe ni wewe Bwana

Mbuyu ni wewe Msingi ni wewe
Ni wewe ni wewe ni wewe hee